• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Balozi wa Indonesia Nchini Tanzania Aihakikishia Simiyu Ushirikiano wa Kibiashara katika Zao la Pamba

Posted on: May 15th, 2018

Balozi wa Indonesia hapa nchini, Prof. Dkt. Ratlan Pardede amesema moja ya malengo makuu ya ziara yake mkoani Simiyu ni kwenda kuona mkoa huo unavyozalisha pamba na kuona namna ya kuongeza ushirikiano kati ya nchi yake na Tanzania(Simiyu) katika biashara ya zao la pamba.

Balozi Pardede amesema hayo wakati wa kikao maalum kati yake na viongozi wa Serikali na baadhi ya wafanyabiashara wa Mkoa huo Mjini Bariadi.

"Nimekuja kuona Simiyu kama mkoa unaoongoza kwa kilimo cha pamba Tanzania, nijue namna mnavyolima, mnavyoichakata, lengo hasa likiwa ni kuongeza kiwango cha pamba inayonunuliwa na nchi ya Indonesia kutoka Tanzania, kwa kuwa nchi yetu inahitaji pamba kwa ajili ya viwanda vya nguo "

Amesema Indonesia inahitaji zaidi ya asilimia 90 ya pamba kama malighafi katika viwanda vilivyopo nchini humo ambayo huagizwa nje ya nchi hiyo, hivyo kutokana na Mkoa wa Simiyu kuwa kiongozi katika uzalishaji wa pamba nchini mkoa huo unaweza kuuza pamba yake nchini Indonesia.

Ameongeza kuwa ili pamba ya Tanzania iweze kununuliwa nchini Indonesia inapaswa kuzalishwa katika ubora unaotakiwa na kuuzwa kwa bei isiyokuwa ya juu zaidi ikilinganishwa na  pamba kutoka katika mataifa mengine yanayozalisha pamba.

Mhe. Balozi ameyataja maeneo mengine ambayo Indonesia itaongeza ushirikiano na Tanzania hususani mkoa wa Simiyu kuwa ni mifugo, miundombinu na umeme hasa unaozalishwa kwa kutumia maji(Hydroelectric Power).

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, amemuomba Balozi Pardede kuwakaribisha wawekezaji kutoka Indonesia kuja kuwekeza mkoani humo katika ujenzi wa viwanda vya nguo(textile industries), huku akiwahakikishia upatikanaji wa ardhi bila malipo yoyote.

Naye Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Ndg. Jumanne Sagini amemuomba Balozi wa Indonesia hapa nchini na Serikali ya Indonesia kuona uwezekano wa kuanzisha mafunzo kwa watumishi wa Simiyu, kuwezesha wafanyabiashara wa Indonesia kushirikiana na wenzao wa Simiyu katika masuala mbalimbali ya kibiashara.

Aidha, Sagini ameomba ushirikiano kati ya Tanzania na Indonesia kuendelea kuimarishwa katika ngazi ya Taifa na kwa Mkoa ambapo ameomba Balozi huyo kuona namna ya kusaidia  Mkoa wa Simiyu kuwa na Mkoa au Mji pacha nchini Indonesia.

Mhe. Balozi Prof. Dkt. Ratlan Pardede yuko katika ziara ya kikazi mkoani Simiyu ambayo inatarajiwa kuhitimishwa Mei 17  mwaka huu

MWISHO

KUPATA HABARI ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI HAPA:-.https://simiyuregion.blogspot.com/2018/05/balozi-wa-indonesia-aihakikishia-simiyu.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa