• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Asilimia 80 ya Wananchi Simiyu kutumia Bima ya Afya

Posted on: March 15th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema mkoa huo umejiwekea malengo ya kuhakikisha zaidi ya asilimia 80 ya wananchi wake kuwa na kadi za bima ya afya ili kujihakikishia upatikanaji wa  huduma za matibabu katika vituo vya kutolea huduma za afya hapa nchini.

Mtaka ameyasema hayo wakati ufunguzi wa Jukwaa la Ushirika Afya wa Mkoa wa Simiyu lililofanyika kwa lengo la kujadili namna wanachama wa Vyama vya Ushirika vya Msingi (AMCOS)wanavyoweza kujiunga na Bima ya afya na kupewa kadi kupitia vyama vyao na kama familia, ambalo limefanyika Machi 14, mjini Bariadi.

Amesema yeye kama Mkuu wa Mkoa atafanya vikao na wanachama wa AMCOS  na makundi mbalimbali ya wananchi katika wilaya zote mkoani hapa na kuzungumza nao kuwaelimisha juu ya umuhimu wa kila mwananchi kuwa na Bima ya Afya kwa ajili ya matibabu.

Aidha, amesema atawaelimisha wananchi juu ya umuhimu wa kuwa katika Vyama vya Ushirika Vya Msingi ambavyo vinawapa nafasi ya kupata matibabu makubwa katika vituo vya kutolea huduma za afya vya binafsi na vya umma kwa gharama nafuu ya shilingi 76,800/= kwa mtu mmoja(mwanachama wa ushirika).

“Nitafanya vikao na wanachama wa AMCOS zote, wakulima, wafugaji, wajasiriamali, makundi yote ya wananchi kwenye mkoa wetu wa Simiyu, tuweze kuwaelimisha faida ya mwananchi wa mkoa wa Simiyu kuwa na bima ya afya, kubwa zaidi umuhimu wa kuwa kwenye ushirika ambao utamwezesha kupata matibabu makubwa kwa bei nafuu” alisema

Katika hatua Nyingine Mtaka amesema katika kipindi cha msimu wa pamba katika kila kituo cha kununulia pamba NHIF itaweka Afisa wake kwa ajili ya kusajili wakulima na wanachama wa vyama vya ushirika walio tayari, hivyo akatoa wito kwa viongozi walioshiriki jukwaa la ushirika afya kutoa taarifa na elimu kwa wenzao juu ya umuhimu wa suala hilo.

Mtaka pia ametoa wito kwa wakulima wote wa pamba kulipa kipaumbele suala la afya kwa kuchukua hatua ya kuwa na bima za afya ili waweze kuona manufaa ya Serikali kuboresha huduma za afya ikiwa ni pamoja na kujenga Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, Hospitali za wilaya kwa kila wilaya na Vituo vingine vya kutolea huduma za afya.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Bernad Konga amesema NHIF ni wadau wakubwa mkoani Simiyu, hivyo wako tayari kutoa huduma bora na wanawafikia wananchi wa makundi yote mkoani hapa na watahakikisha wanatoa kadi za bima ya afya kwa wakati kwa wanachama wote watakaojiunga.

Katika jukwaa hili washiriki wamepata nafasi ya kuchangia michango mbalimbali huku wanachama wa AMCOS wakiunga mkono mpango huo wa kupata bima ya afya kwa gharama ya shilingi 76,800/= ili waweze kumudu gharama za matibabu.

“Mpango huu nimeupokea vizuri ila ninashauri elimu iendelee kutolewa zaidi na zaidi ili wanachama wote wajue umuhimu wa kuwa na kadi za bima ya afya na namna zitakavyowasaidia” Lucas Ephraim mshiriki kutoka AMCOS ya Dutwa Bariadi.

“ Binafsi niko tayari kujiunga na mfuko wa bima ya afya ili nipate hiyo kadi itakayonifanya niweze kutibiwa popote hapa Tanzania, lakini naomba tutakapolipia hiyo 76,800/= kadi zetu tuzipate mapema” Mmoja wa Wanachama wa Vyama vya Ushirika vya msingi, Bw. Magwashi Gandila

Mkoa wa Simiyu una vyama vya Ushirika Vya Msingi(AMCOS) zaidi ya 300 na Jukwaa hili limeazimia wanachama wa AMCOS  wakawe mabalozi wazuri  kuwahamasisha wananchi kujiunga na Bima ya Afya.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/03/asilimia-80-ya-wananchi-simiyu-kutumia.html

Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(katikati) aizungumza na Meneja wa Wanachama kutoka NHIF(kushoto) na Mkurugenzi mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF), Benard Konga, mara baada ya kumalizika kwa Jukwaa la Ushirika Afya Mkoa wa Simiyu lililofanyika kwa lengo la kujadili namna wanachama wa Vyama vya Ushirika vya Msingi (AMCOS) wanavyoweza kujiunga na Bima ya afya na kupewa kadi kupitia vyama vyao na kama familia, ambalo limefanyika Machi 14, mjini Bariadi.

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa