• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Dkt Mwanjelwa Atoa Neno Kambi ya Kitaaluma Kidato cha Nne Simiyu

Posted on: October 6th, 2019

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt Mary Mwanjelwa ametoa wito kwa wanafunzi wa kidato cha nne mkoani Simiyu ambao walipata ufaulu hafifu katika mtihani wa utimilifu (mock) walioko kambi ya kitaaluma ,kutumia fursa hiyo kusoma kwa bidii ili waweze kutimiza ndoto zao.

Dkt Mwanjelwa ametoa wito huo alipowatembelea wanafunzi hao katika kambi ya kitaaluma iliyopo chuo cha ualimu Bariadi mkoani hapa na kuwasisitiza walimu mbali na kuwafundisha masomo ya darasani pia wawafundishe namna ya kukabiliana na maisha baada ya kumaliza masomo ili ambao hawatabahatika kuendelea na masomo ya juu waweze kujiajri na kuajiri wengine.

Katika hatua nyingine Mwanjelwa amewataka wanafunzi kuitumia fursa ya uwepo wao kambini kufanya kile kilichowapeleka, watumie muda mwingi kujifunza na wajiepusha na mahusiano ya kimapenzi ambayo yatawasababishia kushindwa kutimiza malengo yao ya baadaye.

“Maisha bila malengo sio maisha nini matarajio yako baada ya kusoma na endepo hutafaulu ujue namna ya kujiajiri, tumieni fursa ya kuwa hapa kuhakikisha mnasoma kwa bidii ishike sana elimu MUNGU hatakuacha, maisha lazima myatafute ,myatolee jasho, ” alisema Mwajelwa

“Wanafunzi wa kike jitunzeni lindeni utu wenu asitokee mtu akawadanganya mkashindwa kufikia ndoto zenu ninyi ni wa thamani kubwa kumbukeni mbali na mimba kuna magonjwa, ” aliongeza Dkt Mwanjelwa.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini amesema kama mkoa wataendelea kusimamia fedha zote zinazotolewa na serikali ya awamu ya tano  za elimu bila malipo ili ziweze kuleta matokeo chanya .

“Tunatamani kuona elimu bure inayotolewa na serikali inazaa matunda tutapambana kuhakikisha vituo vya kutolea elimu vinakuwa na mazingira bora na kama mlivyomuahidi kwa ziro hakuna na iwe hivyo, ”alisema Sagini

Awali baadhi ya wanafunzi waliopo kambini hapo wamemshukuru mkuu wa mkoa huo kwa kuanzisha kambi za kitaaluma ambazo wamesema zimewawezesha kuwa na uwelewa wa masomo mbalimbali kupitia walimu mahiri hatua iliyowatoa kwenye daraja sifuri mpaka daraja la 111 kupitia mitihani mbalimbali wanayopewa kambini hapo..

“Nilikuja kambini hapa nikiwa na division ziro tulivyofanya mtihani wa mock ufaulu uliongezaka na nikikapata division 111 awali nilikuwa sijui kuandika essay sasa hivi najua na  nina uwezo wa kuandika barua ya kuomba kazi ninachokuhakikishia mhe,pamoja na mkoa chini ya mkuu wetu wa mkoa hatutawaangusha alisema ” Pendo Aguda kutoka shule ya sekondari Old Maswa.

Akiwa kambini hapo Dkt. Mwanjelwa amekabidhi kwa niaba ya Mbunge wa Jimbo la Itilima Mhe.Njalu Silanga kilo elfu moja za unga wa mahindi, kilo mia tano za mchele na mafuta ndoo ishirini kwa ajili wanafunzi walioko kambini.

MWISHO

KUPTA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/10/dkt-mwanjelwa-atoa-neno-kambi-za.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa