• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

RC Simiyu Azindua TTCL Rudi Nyumbani Kumenoga Mkoani Simiyu

Posted on: September 22nd, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amezindua kampeni ya Shirika la Simu Tanzania (TTCL) Rudi Nyumbani Kumenoga mkoani humo na kuipongeza TCCL kwa kuboresha huduma zake na kuwa miongoni mwa mashirika ya Serikali yanayotoa gawio kwa Serikali, fedha ambazo zinasaidia kuboresha huduma za jamii na miundombinu. 

Akizindua kampeni hiyo jana jioni Septemba 21, 2018 Mjini Bariadi, amesema kwa mara ya kwanza TTCL imetoa gawio kwa serikali fedha ambazo sehemu zimewezesha ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ulioanza na Jengo la Wagonjwa wa nje (OPD), ujenzi wa Barabara, miundombinu mingine pamoja na huduma mbalimbali kwa jamii.

Aidha, Mtaka ametoa wito kwa wananchi kutumia huduma za TTCL na kumuomba Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL Bw. Waziri Kindamba kufungua ofisi mkoani Simiyu, kumleta meneja na kuongeza watumishi ili kuongeza wigo wa utoaji wa huduma.

Ameongeza kuwa  Mtendaji Mkuu wa TTCL aimarishe mfumo wa intaneti zaidi ili kuwezesha mpango wa mkoa wa Simiyu wa kufundisha kupitia teknolojia ambapo mtandao wa intaneti utahitajika kwa kiasi kikubwa.

“Tungehitaji tuone wanafunzi wa Simiyu wasome saa 24, wanafunzi wasio na walimu wa kutosha wa sayansi tutajenga vyumba vya madarasa vitakavyowezesha wao kusoma kupitia mfumo wa teknolojia, Mtendaji Mkuu wa TTCL imarisha mtandao wa TTCL wanafunzi wapate intaneti ili tuweze kurahisisha ufundishaji kwenye miji mikuu ya wilaya zetu” alisema.

Wakitoa maoni yao huduma za TTCL baadhi ya wananchi wa Mkoa wa Simiyu wamesema walikuwa hawazitumii lakini baada ya shirika hilo kuboresha huduma zake hasa za mtandao wa intaneti wameanza kuzitumia na wakaomba ziendelee kuboreshwa zaidi.

“ Mimi nilikuwa sijawahi kutumia mtandao wa TTCL nilikuwa natumia mitandao mingine tu lakini nilivyoona matangazo nikasema ngoja nijaribu, nikaenda kununua laini na kuanza kutumia, napenda kutumia zaidi intaneti yao  iko vizuri” alisema Emmanuel Elias mkazi wa Bariadi

Naye Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL Bw. Waziri Kindamba ametoa wito kwa Watanzania wote kurudi nyumbani na kuendelea kutumia huduma za TTCL kwa kuwa kadri wanavyotumia huduma hizo wanazalisha faida ambayo itaendelea kutumika hapa nchini kwa maendeleo ya nwananchi na Taifa kwa ujumla.

Aidha, kutokana na Taarifa ya kuwa na siku nne za maombolezo kwa Taifa ililotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kufuatia ajali ya Kivuko cha MV Nyerere huko Ukerewe Mkoani Mwanza, Mkurugenzi Kindamba amesema TTCL haitaendelea na kampeni hiyo RUDI NYUMBANI KUMENOGA mpaka siku hizo zipite ili kuungana na Watanzania wengine kuomboleza juu ya msiba huu wa Taifa.

“Mhe. Rais ametangaza siku nne za maombolezo kuanzia Septemba 21 hadi Septemba 24, 2018 kufuatia ajali ya kuzama kwa Kivuko cha MV Nyerere, tulikuwa tumepanga kuanza na Simiyu, twende Kahama halafu Tabora lakini kwa sababu ya msiba huu uliotugusa Watanzania wote na kwa kuwa  Shirika hili ni la Watanzania na sisi tumeguswa hivyo itabidi shughuli hii tuisitishe kwa muda; Mungu awarehemu wenzetu waliotangulia na majeruhi wapone haraka” alisema.

MWISHO

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Orodha ya Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2020 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 07, 2019
  • Matokeo ya Kidato cha NNe mwaka 2018 January 24, 2019
  • Fungua

Habari Mpya

  • RC Simiyu Asitisha Leseni Za Uchimbaji Madini Mgodi wa Lubaga

    December 17, 2020
  • Waziri wa Kilimo Prof. Mkenda, Naibu Waziri TAMISEMI Dkt Dugange Wanogesha RCC Simiyu

    December 16, 2020
  • TANROADS Simiyu Kutumia Bilioni 11.4 Ujenzi wa Barabara na Madaraja

    December 16, 2020
  • Viongozi, Wananchi na Wadau Simiyu Watakiwa Kushirikiana Kukamilisha Ujenzi wa Madarasa

    December 13, 2020
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa